|
Written by M. M. Mwanakijiji
|
|
Sunday, 30 May 2010 |
|
Mzee Pwagu wa kundi la Pwagu na Pwaguzi amezikwa leo JIjini Dar na mamia ya waombolezaji ambao bado wanakumbuka burudani ya pekee aliyoweza kuitoa katika maisha yake kwa mamilioni ya Watanzania kufuatia kudumu katika burudani ya maigizo na vichekesho radioni kwa miaka mingi.
 Aliyekuwa msanii mkongwe wa maigizo hapa nchini, Rajabu Hatia ‘Mzee Pwagu’ jioni hii amezikwa kwenye makaburi ya Kigogo CCM jijini Dar es Salaam baada ya kufariki duania jana kutokana na ugonjwa wa kwikwi aliokuwa akitibiwa katika Hospitali ya Amana jijini Dar. Mazishi hayo yalihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wasanii wa filamu na maigizo. Pichani, Mzee Magali akiwa na jeneza lenye mwili wa marehemu wakati akiwaongoza waombolezaji kuelekea makaburini.
 Safari nya makaburini.  Mzee Small (kushoto) na Kingwendu wakiwa msibani hapo.  Msanii wa kundi la Comedy Orijino, Joti (kushoto) akiwa na wasanii wenzake Swebe na Mzee Magali (kulia) wakibadilishana mawazo msibani.  Bi. Mwenda (kushoto) akiongea jambo na waombelezaji.  Mwili wa marehemu ukiingizwa kaburini.  Waombolezaji wakifukia mwili wa marehemu.  Marehemu Rajabu Hatia ‘Mzee Pwagu’
PICHA: RICHARD BUKOS /GPL
|