|
Written by DarHotWire
|
|
Thursday, 08 November 2007 |
|
Wakazi wa Manispaa ya Iringa mkoani hapa, kesho wanatarajiwa kupata burudani ya aina yake wakati wakali wa vichekesho Ze- Comedywatakapotumbuiza kwa pamoja katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini hapa. Mratibu wa tamasha hilo, Edo Bashir, alisema kuwa maandalizi yote yanakwenda vema na yamekwisha kamilika na pia kutakuwa na ulinzi mkali siku ya kesho. Bashir alisema lengo la onyesho hilo, lililoandaliwa na Radio Ebony FM ya hapa, kwa ushirikiano na kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom, ni kutaka kukutana na wasikilizaji wa radio hiyo na kupata maoni.
|
|
Last Updated ( Monday, 13 October 2008 )
|