|
Aliyempiga picha ya uchi mtoto wa shule adai "nilipitiwa na shetani" |
|
Written by M. M. Mwanakijiji
|
|
Wednesday, 12 August 2009 |
ASKARI anayetuhumiwa kuwapiga picha za uchi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kurasini Dar es Salaam na mama mjamzito mwishoni mwa wiki amejitokeza na kukiri kosa na kuwaomba radhi walalamikaji kwa maelezo kwamba alipitiwa na shetani. Akizungumza na gazeti hili jana kituo cha Polisi Barabara ya Kilwa askari huyo alisema alikifanya kitendo hicho kwa bahati mbaya na hakuwa na nia yoyote ile mbaya kwa mwanafunzi huyo na mjamzito huyo.
"Sikuwa na nia mbaya ila shetani tu aliyenipitia hivyo nawaomba walalamikaji wangu anisamehee kwa yote yaliyotokea, nipo tayari tulizungumze kiubinadamu."alisema askari huyo.
Katika hatua nyingine, mama mzazi wa mwanafunzi huyo Bi. Bernadeta Fatael mbaye alifika kituoni hapo kwa mara ya kwanza tangu kutokea tukio hilo, alisema siku hiyo hakuwepo alikuwa katika mihangaiko yake
Alisema kuwa kutokana na baba mkubwa wa mwanafunzi huyo kwenda kazini jana ilimlazimu kwenda kituoni hapo ili kujua hatima ya kesi hiyo.
Bi. Bernadeta, alisema kuwa baada ya kufika kituoni hapo mpelelezi wa kesi yao alimwambia kuwa asubiri kidogo ili naye aende kutoa maelezo yake.
"Muda kidogo waliniita ndani nilipoingia waliniuliza jina langi kisha kuanza kunihoji na walipomaliza waliniambia niweke saini karatasi ile,"alisema.
Kabla ya kutia saini alimuomba mpelelezi huyo kumsomea ili ajue nini kilichoandikwa.
"Mwanzo wa maelezo alisoma kile alichokuwa ananihoji lakini mwishoni nilishituka baada ya kuandika kuwa nikiwa kama mwakilishi wa upande wa wazazi tulikaa na kuafikiana kumsamehe askari huyo kitu ambacho sikukisema,"alisema mama huyo.
Baada ya kugundua njama hizo alimuita mlalamikaji mwingine ambaye mke wake naye alipigwa picha hizo, Bw. Frank Kazimili ambapo alimwambia askari huyo kitendo anachotaka kukifanya ni kinyume na sheria na ni njama za kutaka kumsaidia askari huyo.
"Haiwezekani kabisa kwa nini amuite huyu mama pekee yake wakati walalamikaji wote tupo hapa na kitendo cha kutaka kumsainisha bila kutushirikisha na kusema kuwa tumemtuma sisi kama walalamikaji kuwa tumefikia muafaka wa tunamsamehe ni uongo na mpelelezi huyu hatumtaki hatuna imani naye,"alisema Bw. Kazimili.
|