MwanaKijiji.COM

Monday
May 21st
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home arrow National arrow Lake Zone arrow Padre auawa Maswa
Padre auawa Maswa
(0 votes)
Written by Mwananchi   
Saturday, 19 January 2008
WATU wanaodhaniwa kuwa majambazi, wanadaiwa kumuua kwa kumpiga nondo kichwani na risasi katika mguu wake wa kushoto, Padri Angelo Nkuba wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Sayusayu wilayani hapa Mkoa wa Shinyanga baada ya kuvamia kwenye makazi yao.

Habari kutoka katika eneo la tukio zinadai kuwa, Padri huyo alifia njiani wakati akikimbizwa katika Hospitali ya Wilaya Maswa kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Kabla ya kifo hicho, juzi majira ya saa 2.30 usiku wakati padri huyo, akiwa na wenzake wawili, Padri Shija na Padri Masanja katika makazi hayo, wakila chakula cha jioni, walivamiwa na majambazi hayo na kuwateka.

Majambazi hayo yaliyokuwa na nondo na bunduki na kwamba baada ya kuwateka mapadri hao, waliwafungia katika chumba kimoja ambacho kinachotumika kama stoo na kumwamuru Padri Angelo awapatie pesa.

Kisha yalimchukua padri huyo hadi katika chumba chake cha kulala na walipopatiwa pesa, walidai hazitoshi na kuamua kumpiga kichwani kwa nondo na risasi tatu katika mguu wake wa kushoto.

Baada ya kumjeruhi yalitoweka katika eneo la tukio wakitumia gari ambalo walikuwa wamelificha pembeni mwa makazi ya mapadri hao.

Polisi wilayani hapa, wamethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kusisitiza kuwa, wanaendelea kuyasaka majambazi hayo.

Comments (0)add comment

Write comment

busy
Last Updated ( Tuesday, 28 October 2008 )
 
Ni nani anafaa kuingoza Tanzania kama Rais kuanzia 2010-2015?
 

Photo Albums

Just $6.95/Mo
Unlimited Space, Unlimited Transfer, Free Domain
www.bluehost.com

MwanaKijiji.COM LIVE

Window Player   RealAudioPlayer   Itune Player