| Michango ya awali yapokelewa |
| Written by M. M. Mwanakijiji | |
| Saturday, 16 January 2010 | |
Tulipoanza harambee hii ya kuwachangia ndugu zetu walioathirika na mafuriko kuna watu walidhania tunatania au ni mzaha. Hatuwezi kuwasubiri Wamarekani na meli zao kuja kutusaidia kwenye vitu ambavyo sisi wenyewe tuna uwezo nao. Jana (Ijumaa) michango ya awali imewasilishwa kwa Chama cha Msalaba Mwekundu na Mlezi wa TPN Dr. Maua Daftari kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Msalaba Mwekundu nchini Mstahiki Alhaji Adam Kimbisa (Dar-es-Saalam).
zaidi ya wadau 1,200 wachangia harambee ya waathirika wa mafuriko kilosa, awamu ya kwanza ya michango yakabidhiwa msalaba mwekundu Mlezi wa Mtandao wa wanataaluma (Tanzania Professionals Network - TPN) Dk. Maua Daftari (shoto) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, akimkabidhi Katibu Mkuu wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Tanzania na Meya wa Jiji la Dar, Alhaj Adam Kimbisa, msaada wa vitu mbali mbali vyenye thamani ya shilingi 1.4m/- vilivyotolewa na wadau baada ya kuhamasishwa na Jamii Forum, Globu ya Jamii, TPN na mwanakijiji.com kusaidia waathirika wa mafuriko huko Kilosa katika sherehe fupi iliyofanyika jana jioni ofisi za Msalaba Mwekundu jijini. Wengine wanaoshuhudia toka shoto ni Rais wa TPN Mzalendo Sanctus Mtsimbe Katibu Mkuu wa Chama cha Msalaba Mwekundu na Meya wa Jiji la Dar Alhaj Adam Kimbisa akimshukuru Dk. Maua Daftari baada ya kupokea mchango wa pesa taslimu wa shilingi milioni moja na elfu 68 na senti 80 zilizochangwa na wadau mbalimbali duniani kusaidia waathirika wa mafuriko huko Kilosa. Picha zingine na maelezo ya namna ya kuchangia ndugu zetu ---------------------- Globu ya Jamii kwa kushirikiana na TPN, http://www.jamiiforums.com/ na www.mwanakijiji.com tunatoa shukrani za dhati kwa wale wote waliojitolea kuchangia ndugu zetu walioathirika na mafuriko huko Kilosa, mkoani Morogoro. Msaada ni msaada tu, hauna udogo wala ukubwa, muhimu ni tendo (gesture) ya kuguswa na matatizo ya wenzetu na kuamua kusaidia. Michango inaendelea kupokelewa na si lazima iwe ni pesa taslimu bali hata misaada ya mablanketi, vyakula na maji, madawa, nguo, viatu na kadhalika. Bofya hapo juu kujua namna ya kufikisha msaada wako huku ukikumbuka kwamba kutoa si utajiri. Inawezekana: Watanzania KWA Watanzania Harambee ya Mafuriko Kilosa ------------------------------------ Email:
This e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it
9: Unaweza kuchangia vile vile kwa kupitia mtandao wetu huu wa mwanakijiji.com hapo juu mahali panaposema "Donate" na unaweza kutumia kadi yoyote ya kibenki katika njia salama. Au kama una Paypal tumia anuani klhnews(#)klhnews.com
Set as favorite
Bookmark
Email This
Comments (0)
![]() Write comment
|