MwanaKijiji.COM

Wednesday
Feb 08th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home arrow National arrow Taifa arrow Polisi Ichunguzwe kifo cha WP Susan
Polisi Ichunguzwe kifo cha WP Susan
(2 votes)
Written by M. M. Mwanakijiji   
Wednesday, 07 July 2010
HojaMaelezo ambayo yamekuwa yakitolewa hadi hivi sasa juu ya kifo cha WP Susan huko Tarime kwanza hayaingii akilini na yana dalili ya jaribio la makusudi la uongozi wa Polisi kujaribu kuficha kilichotokea. Maelezo ya awali ya kifo cha dada huyo ambaye inadaiwa kuwa alirudishwa kituoni baada ya kuuongoza vibaya msafara wa Rais na hata kutakiwa kuwekwa rumande. Maelezo yote kwanza hayakubaliani kabisa na mtu yeyote anayejua utaratibu wa kazi wa Polisi linapokuja suala la mtuhumiwa wa kosa lolote na hasa kwenye masuala ya court martial. Ukiangalia video ya maelezo ya tukio hilo kama ilivyotolewa na IGP Mwema utaona kuna kitu ambacho hakiko sawa.

Kutokana na mgongano wa maelezo ambayo yametolewa toka awali na maelezo ambayo yameendelea kuvuja hadi hivi sasa inaonekana kuna mtu hasemi ukweli. NI masikitiko yangu kuwa Jeshi la Polisi linaachwa kujichunguza lenyewe hasa tukizingatia kuwa suala hili linagusa chombo zaidi ya Polisi kwani taarifa za awali zilidokeza kuwa binti huyo alinyanyaswa na watu wa Usalama wa Taifa.

 Ili haki itendeke Natoa wito kwa Tume ya Haki za Binadamu au chombo kingine huru kifanye uchunguzi angalau kwa mambo makubwa matatu:

a. Mazingira ya WP Susan kurudishwa kituoni, nani alitoa agizo gani na kwa mamlaka gani aliyonayo.

b. Kujua utaratibu wa kumrudisha kituoni kwa kosa kama hilo ni upi na kama ulifuatwa.

c. Kufahamu kwanini silaha zimewekwa kiholela kituoni hadi kuweza kuchukuliwa na mtu ambaye hakuwa anatakiwa kuwa na silaha - taratibu gani za kijeshi zilikiukwa.

d. Ni nani mwingine alikuwepo ndani ya ofisi ya mkuu wa kituo ambako inadaiwa Susan alikimbilia? Nini kilimtisha hadi kutaka kuchukua silaha hasa ikizingatiwa kuwa suala la kukosesha msafara wa kiongozi siyo kosa kubwa ambalo linaweza kutishia ajira ya mtumishi, kwani imeshawahi kutokea huko nyuma kwa mapolisi wengine bila kuwa jambo la kutisha hadi kumfanya mtu ajisikie maisha hayana thamani.

e. Uongozi wa Jeshi la Polisi umehusika vipi kuficha habari sahihi au za ukweli au kwa makusudi kujaribu kuonesha kuwa binti huyo ndiye wa kulaumiwa na ni yeye pekee.

 

Tunachosema tunataka wote wanaohusika na kifo cha binti huyu afisa wa Jeshi lazima wawajibishwe mara moja. 

Comments (2)add comment
Kama : ...
Mwanakijiji hapa tunatakiwa kufanya mabadiliko ya muda mrefu na muda mfupi katika majeshi yetu yote hasa Usalama wa Taifa, Magereza, Uhamiaji na Polisi. Kwenye jeshi la polisi matukio tata yamekuwa mengi na pia kinachofanyika kujaribu kuwalinda ma kuwaficha wahalifu kwa kuwahaisha vituo vya kazi na matukio yanaongezeka na picha halisi ya jeshi la Polisi inabaki kuwa tata...

Hivi jeshi letu la polisi wanapokesewa wanachunguzwa na nani kama taasisi huru...Sidhani kama kuna chochote kipo mahali katika kufuatilia matukio kama ya kifo cha huyu polisi...
Tuache kuweka viraka katika nguo chakavu kama tunataka kuwa na jeshi la polisi la kisasa basi tunahitajika kuwawajibisha wanaokosea kwa mujibu wa sheria zilizopo na pia kufanya tathmini ya hizo sheria kutokana na matukio...
1

July 07, 2010
Votes: +0
Guadalupe23Carson: ...
All people deserve very good life time and mortgage loans or just secured loan can make it much better. Just because people's freedom relies on money state.
2

July 12, 2010
Votes: +0

Write comment

busy
Last Updated ( Wednesday, 07 July 2010 )
 
Ni nani anafaa kuingoza Tanzania kama Rais kuanzia 2010-2015?
 

Photo Albums

Just $6.95/Mo
Unlimited Space, Unlimited Transfer, Free Domain
www.bluehost.com

MwanaKijiji.COM LIVE

Window Player   RealAudioPlayer   Itune Player