HOJA ya mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe ya kutaka serikali itaifishe mitambo ya kuzalisha umeme ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited, imevuta hisia tofauti huku serikali ikisema haitaweza kuitekeleza kwa kuwa haina sera ya utataifishaji. Kauli ya serikali imekuja siku moja baada ya Zitto kuwaambia waandishi wa habari kuwa serikali haina budi kufumba macho na kutaifisha mitambo hiyo ya Dowans ili kuiondoa nchi katika janga kubwa la ukosefu wa umeme linaloongeza ugumu wa maisha kwa wananchi na kuiingizia serikali hasara kubwa.