|
Bunge lavunjwa; kinyang'anyiro cha uchaguzi kuanza |
|
Written by M. M. Mwanakijiji
|
|
Friday, 16 July 2010 |
Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg. Jakaya Mrisho Kikwete amevunja Bunge leo hii kuashiria kuanza kwa mchakato wa kuelekea uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba mwaka huu. Akihutubia Bunge hilo la tisa kwa takribani masaa mawili na robo Rais Kikwete ameanisha yale ambayo ameyaelezea kuwa ni mafanikio ya serikali ya ngwe ya kwanza ya awamu ya nne huku akiahidi kuwa machache ambayo yaliahidiwa lakini hayajakamilishwa yatakamilishwa endapo wananchi watakipa chama chake nafasi nyingine ya kuliongoza Taifa.
Sehemu ya hotuba hiyo ya Rais Kikwete itapatikana katika mtandao wetu wa http://www.youtube.com/mwanakijiji na vile vile katika maandishi katika "facebook.com/mwanakijiji" Akihutubia ukumbi ambao leo ulikuwa umefurika karibu wabunge wote Rais Kikwete alielezea kwa urefu jinsi serikali yako ilivyofanikiwa kuongeza wingi wa vitu mbalimbali ambavyo viliahidiwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM. Pamoja na kuwashukuru wananchi Rais Kikwete alishukuru vyombo na taasisi mbalimbali ambazo kwa kiasi na namna yao ziliweza kuchangia katika kufanikisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za serikali.
|