MwanaKijiji.COM

Wednesday
Feb 08th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home arrow Siasa arrow Siasa arrow Sabodo aichangia CHADEMA milioni 100!
Sabodo aichangia CHADEMA milioni 100!
(1 vote)
Written by Mwandishi Maalum   
Monday, 12 July 2010
ImageKatika kuonesha ukomavu na uthubutu wa kisiasa mfanyabiashara biashara mkubwa nchini Bw. Mustaffa Jaffari Sabodo ametoa hundi ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya kukisaidia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) huku akiahidi kuwa ataendelea kufanya hivyo katika siku za mbeleni. Katika tukio hili la kihistoria katika vyama vya kisiasa nchini Bw. Sabodo alitoa hundi hiyo mbele ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema Bw. Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Wilbroad Slaa. Bw. Sabodo ambaye amekiri kuwa yeye ni mwana CCM amesema mchango wake huo ni katika kutambua mchango wa CHADEMA katika kutetea maslahi ya taifa na uongozi wao wa kuhoji masuala muhimu huko Bungeni.

“Mimi ni mwanachama wa CCM lakini napenda kuona demokrasia ikikua huku kambi ya upinzani ikiimarika kwa kuwa na wabunge wengi bungeni ili kushamirisha maendeleo nchini……na nawachangia CHADEMA kwa kuwa natambua umakini wenu katika siasa za hapa nchini na hasa Bungeni”, Alisema.

Bw. Sabodo amesema kuongezeka kwa wabunge wa upinzani bungeni ni jambo la muhimu katika kutoa upinzani kwa CCM na kusukuma maendeleo ya wananchi huku akikitaka CHADEMA kuongeza nguvu zaidi katika harakati zake za kisiasa na kumwelezea Dr Slaa kuwa ni mwanasiasa mwenye uchungu wa kweli na watanzania.

http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/politics/dsc09389_phixr.jpg

 

Aidha Bw. Sabodo amesema ana mpango wa kuichangia fedha zaidi CHADEMA ili kuimarisha harakati zake za kisiasa na kuahidi kufanya hivyo atakaporejea nchini akitokea India kwenye matibabu.

Akizungumza katika makabidhiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwa Bw. Sabodo Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam Mwenyekiti  wa CHADEMA Freeman Mbowe ameshukuru na kutaja msaada huo kuwa ni wa kihistoria katika siasa za vyama vingi nchini.

Amesema mara nyingi imekuwa ni vigumu kwa wafanyabiashara wakubwa wa kada ya Bw. Sabodo kuchangia kwa uwazi tena kiasi kikubwa cha fedha na kutaka hatua hiyo kuigwa na wafanyabiashara wengine nchini.

“Kwa kweli tunashukuru sana hii ni historia mpya katika siasa za vyama vingi nchini, ni wajibu wa wafanyabiashara wakubwa kuona umuhimu wa kusaidia vyama vyote makini nchini bili kuwa na ubaguzi wala woga, Mzee ameonyesha njia naamini itakuwa ni mfano kwa wengine wenye uwezo, Alisema Bw. Mbowe.

 http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/politics/dsc09396_phixr.jpg

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Dr Slaa ameshukuru kwa mchango huo na kudokeza kwamba mchango utatumika kwa kadiri ya vipaumbele vitakavyopangwa kwenye Kamati Kuu ya chama inayotarajiwa kufanyika tarehe 20 Julai 2010 ikilenga zaidi katika kutekeleza mipango endelevu ya kuimarisha chama kama Operesheni Sangara na utekelezaji wa mikakati ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

“Nawaomba watanzania wengine wa kada na uwezo mbalimbali kuichangia CHADEMA ili kuondokana na ukiritimba wa chama kimoja kwani ni hatari kwa maendeleo na usalama wa nchi kama michango yote ikielekezwa kwa chama tawala pekee. Natoa mwito kwa vyombo vya dola kuacha kuwatisha watanzania wenye mapenzi mema wanaochangia vyama mbadala kama CHADEMA kwani kufanya hivyo ni kuhujumu taifa na kukwamisha maendeleo  ya nchi”

Comments (2)add comment
proches: ...
hii inadhihirisha ni kwa kiasi gani demokrasia imekuwa hapa nchini... imekuwa vigumu sana kuona watu wenye nafasi katika jamii yetu wakithubutu kujihusisha na siasa za upinzani. nadhani wengi wanaowasaidia wapinzani hufanya hivyo kwa kificho labda kwa kuwa wanaogopa kuandamwa baadae na vyombo vya dola.
upinzani unajenga demokrasia ya kweli na ni vyema wapinzani nao wasaidiwe ili waweze kutekeleza wajibu wao bungeni kwa kukosoa serikali pale inapokosea. watu waache woga... tufuate mfano huu wa Bw. Sabodo kuthamini mchango wa wapinzani. hata rais wetu Mheshimiwa Kikwete ameonesha kuwathamini wapinzani kwa kuwaalika kwenye mkutano mkuu wa CCM uliomalizika hivi karibuni.
1

July 14, 2010
Votes: +1
Mjivuni: ...
Kwanza naomba nijitambulishe kuwa mimi sio mwanachama wala mshabiki wa chama chochote ni mwananchi mpenda nchi.

Pili huyo Bw Sabodo napenda kumpongeza kwa ujasiri wake maana matajiri wa nchi yetu ni wa upande mmoja ili waonekane kwenye kurasa zambele za magazeti na Luninga.

Lakini la tatu napenda kutahadharisha isijekuwa ni mtego wa pesa za kifisadi ili baadae ujumbe utafsiriwe vingine. upokeeni kama mtazamo wangu. juu ya kuamini viongozi wa hicho chama kilichopewa msaada pia ni werevu.
2

August 04, 2010
Votes: +0

Write comment

busy
Last Updated ( Monday, 12 July 2010 )
 
Ni nani anafaa kuingoza Tanzania kama Rais kuanzia 2010-2015?
 

Photo Albums

Just $6.95/Mo
Unlimited Space, Unlimited Transfer, Free Domain
www.bluehost.com

MwanaKijiji.COM LIVE

Window Player   RealAudioPlayer   Itune Player