|
Tanzania Oyee!! Taifa Stars 1, Ivory Coast 0 |
|
Written by M. M. Mwanakijiji
|
|
Wednesday, 25 February 2009 |
Kibarua cha kocha wa timu ya Taifa ya Ivory Coast kinaelekea kuota nyasi baada ya timu kamambe ya Taifa Stars ya Tanzania kuibanjua timu yake bao moja bila katika michuano ya kwanza ya timu za Taifa za wachezaji wa ndani (CHAN) inayofanyika huko Ivory Coast. Bao hilo la Tanzania lilifungwa kwa gonga moja ya kichwa ya mshambuliaji machachari Mrisho Ngassa(pichani kushoto). Timu ya Tanzania ikicheza kwa kujiamini chini ya kocha wake Mbrazili Maximo iliweza vyema kulinda bao hilo liliopatikana dakika ya 38 ya mchezo huo. Kwa ushindi huo timu hiyo ya Tanzania imejiweka katika nafasi nzuri ya kuendelea na mashindano hayo.
Mechi hiyo ambayo dakika za mwisho zilitafsiriwa na mashabiki wa Tanzania kama jitihada za refarii kuibeba Ivory Coast ilikuwa ni ya kusisimua na yenye mvuto wa aina pekee ambapo timu hiyo changa ya Tanzania imezidi kujijengea jina katika eneo la Afrika ya Magharibi.
|
|
Last Updated ( Thursday, 26 February 2009 )
|