Wamemdharau Nyerere na Kuivunja Misingi sasa hawana pa kushikilia!
WAMEMDHARAU NYERERE NA KUIVUNJA MISINGI - HAWANA PA KUSHIKILIA Kwao Nyerere siyo "Baba wa Taifa" tena; kwao ni "Mzee Nyerere"; kwa watawala wetu hawa walioshindwa wanasema wamefanya mambo mengi sana ya maendeleo kkuliko "Wakati wa Nyerere". Wanajitamba kuwa wao wamekuza sana demokrasia na kuwa hata "Nyerere" hakuweza kufanya waliofanya wao. Katika upotofu wao wanaamini kabisa kuwa wao wanapendwa zaidi; na wanapendwa kwa sababu wamefanya mengi mno na hawaelewi kwanini watu hawaoneshi shukrani! Ndio maana kila kukicha hawaachi kubembeleza kwa wananchi kuwa "hamuoni tunayofanya" na kuwa watu wanalaumu tu lakini hawatoi pongezi kwa "mazuri mengi". Imefika mahali Kikwete mwenyewe amedai mahali fulani anataka kukumbukwa kuwa ni "bwana maendeleo"; anasema hivi kwa sababu anapokaa ofisini anaamini kabisa kuwa ameweza kuwapatia Watanzania 'vitu" vingi sana vya maendeleo kuliko wakati wowote wa historia - vitu ambavyo hata Nyerere hakuweza kuwapatia. Kikwete anataka awe juu ya Nyerere kwa … [Soma Zaidi...]
Somo kwa Watawala: Serikali haiko Juu ya Wananchi
Tunachoshuhudia Mtwara ni tatizo la serikali au watendaji wa serikali kutokuelewa ile 'supremacy of the people'. Kuna hisia au mawazo kuwa serikali iko juu ya wananchi; hivyo inaweza kufanya lolote, popote, kwa yeyote na kwa lolote. Sasa wananchi wanapojitokeza kukataa serikali inaona imedharauliwa na nguvu zake zimebezwa; haijiulizi kwanini wananchi wanakataa na kama kweli wanakataa … [Soma Zaidi...]
Yaliyojiri Mtwara Leo – Kukasirika kwa Wananchi na Nguvu ya Watawala
Hadi siku itakapokishwa mengi yatakuwa yamesikiwa: Kutoka katika tovuti ya Mtwara Kumekucha habari zifuatazo kuhusiana na mwamko wa kupinga bomba la gesi ambao umeibuka tangu mwishoni mwa mwaka jana. Machafuko yanaendelea na inaonekana serikali ya CCM haijapata bado jibu la kuridhisha kwa wananchi zaidi ya kuamua kutumia nguvu kuzima mwamko huo. Huko MIKINDANI ofisi zote za serikali zavamiwa … [Soma Zaidi...]
Swali la Ugomvi: Serikali ikipiga marufuku mitandao ya kijamii Tanzania utakubaliana nayo?
Swali la uchochezi: Je utafanya nini kama Serikali ya Tanzania ikiamua kuzuia mtandao wa Facebook, Twitter, Youtube na JamiiForums kutumika nchini (Walioko Tanzania wasiweze kuipata) ili kudumisha amani, umoja na utulivu na kuondoa uchochezi kwa vile mitandao hiyo inadaiwa "kuandika mambo ya uchochezi na kuchafua viongozi na serikali ya CCM"? … [Soma Zaidi...]
Wamachinga wasifukuzwe mijini!
Kwanini serikali (manispaa mbalimbali) zinajitahidi sana kuwakufuza wamachinga mijini? Tumeona haya Dar, Mwanza, na sasa Iringa; na tumeona pia Arusha. Hivi hawa wanaofanya hivi hawajafika kwenye miji mikubwa duniani ambapo nafasi ya wafanyabiashara ndogondogo ni sehemu ya mfumo wa uchumi wa mji? Ni kweli hakuna mtu anayefikiria namna ya kuwaaccommodate wamachinga katika majiji yetu? Kwanini … [Soma Zaidi...]
Wimbo Niupendeao- Bushoke “Dunia”
Naamini mojawapo ya nyimbo za kuvutia sana na ambazo ala zimecharazwa vizuri, beti zimepangwa zikapangika na kuthibitisha kuwa Bushoke ni miongoni mwa waimbaji (vocalist) wa kizazi chake. Sauti yake inanikumbusha sana ya Zico Zengekala! BUSHOKE DUNIA NJIA http://www.youtube.com/watch?v=aqFJ_Uccqmc … [Soma Zaidi...]